• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Benki ziko tayari kufadhili sekta ya mafuta na gesi

    (GMT+08:00) 2019-10-09 19:08:04

    Benki zimeonyesha nia ya kufadhili miradi kadhaa ambayo inatekelezwa chini sekta ya mafuta na gesi Uganda kwa sababu inaweza kuleta faida.

    Gharama za miradi mbalimbali inayohitaji ufadhili ni takriban $751 milioni.

    Akizungumza wakati wa Mkutano wa Ufadhili wa Sekta ya Mafuta na Gesi kupitia mnyororo wa thamani katika Hoteli ya Serena mjini Kampala jana,Mkuu wa Biashara na Mnyororo wa Ugavi katika Benki ya Absa,Bw David Mparutsa,alisema Absa Group iko tayari kufadhili kampuni za ndani zinazoshiriki katika mnyororo wa thamani wa mafuta na gesi.

    Mparutsa alisema Absa ina jukumu kubwa katika sekta ya mafuta na gesi na imetoa rasilimali zake nyingi katika miradi mbalimbali barani Afrika.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako