Klabu ya Mpira wa wavu ya Gisagara imeanza maandalizi mapema kujiandaa na ligi ya taifa ya mpira wa wavu mwaka 2019/2020 ambayo itaanza kutimua vumbi Novemba 9. Mabingwa hao mara mbili, ambao msimu uliopita walimaliza nafasi ya pili, wameapa kurejesha ubingwa wao baada ya hivi karibuni kumsaini mshambuliaji wa kulia Lawrence Yakan Guma na Mganda Malinga Kathbart. Kwenye mahojiano na Times Sport kocha wa Gisagara Pierre Marshal Kwizera amesema klabu yake inalenga kuchukua taji la ligi katika msimu ujao, lakini pia wanataka kuchukua mataji ya michuano yote watakayoshiriki wakianzia na mashindano ya kabla ya msimu yanayofanyika Novemba 2 na 3.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |