• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Reli ya kisasa iliyorefushwa nchini Kenya kuhimiza ukuaji wa viwanda na kuhimiza nguvu ya ushindani

    (GMT+08:00) 2019-10-16 08:52:26

    Mtaalamu amesema, reli ya kisasa ya SGR inayounganisha Nairobi na kaunti ya kitalii ya Naivasha itachochea ustawi wa viwanda na kuongeza nguvu ushindani ya bidhaa za Kenya katika nchi za nje.

    Mhadhiri wa uchumi kutoka chuo kikuu cha Nairobi Bw. Garrison Ikiara, amesema uzinduzi wa sehemu ya pili ya reli ya SGR utahimiza uchumi wa Kenya kupitia usafirishaji wa bidhaa kwa maeneo ya ndani na kote nchini humo.

    Bw. Ikiara amesema moja kati ya faida za moja kwa moja zinazotokana na uendeshaji wa reli kutoka Nairobi hadi Naivasha, ni kupunguzwa kwa kiasi kikubwa kwa mizigo inayosafirishwa kutoka bandari ya Mombasa hadi nchi mbalimbali ikiwemo Uganda, Sudan Kusini, Rwanda, DRC na Ethiopia.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako