Mamlaka ya afya ya Malawi imekanusha ripoti za uwongo kwamba mtu mmoja amegunduliwa kuwa na Ebola kwenye eneo la Karonga linalopakana na Tanzania. Hofu hiyo ilitokea Jumapili wakati wafanyakazi wa afya kwenye eneo hilo waligundua mwanamume mwenye umri wa miaka 37 kuwa na dalili za Ebola. Ofisa wa afya wa nchi hiyo Bw. Louis Tukula amesema mtu huyo alikuwa na maambukizi ya bakteria na si Ebola.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |