• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa China atoa wito wa amani na urafiki katika michezo ya kimataifa ya majeshi

    (GMT+08:00) 2019-10-18 20:41:16

    Rais Xi Jinping wa China leo amekutana na viongozi wa idara za ulinzi na majeshi ya nchi zinazoshiriki kwenye michezo ya kimataifa ya majeshi, na maofisa wa Kamati ya Kimataifa ya Michezo ya Majeshi, kabla ya kuanza rasmi kwa michezo hiyo.

    Rais Xi Jinping amesema, kauli mbiu ya michezo hiyo kwa mwaka huu ni "Ukuu wa Majeshi, Amani ya Dunia" inaonesha matarajio kuwa wachezaji kutoka nchi mbalimbali wataonesha dhamira imara ya michezo na nguvu ya michezo katika kuondoa kivuli cha vita na kujenga mawasiliano kati ya tamaduni tofauti.

    Rais Xi amewataka askari kushindana kwa usawa na kuwezesha mawasiliano na kujifunza tamaduni tofauti za kijeshi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako