Tume ya Umoja wa Mataifa inayochunguza makubaliano ya kusitisha mapambano mjini Hodeidah, Yemen imeanza kujenga vituo vya uchunguzi kwenye mistari ya mbele ya vita mashariki na kusini mwa mji huo, ili kuzuia mapambano kati ya vikosi vya serikali na waasi wa Houthi. Makubaliano ya kusimamisha mapambano yalifikiwa mjini Stockholm mwishoni mwaka jana, na kuchukuliwa kama ni hatua ya mwanzo kumaliza vita ya wenyewe kwa wenyewe nchini Yemen.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |