Mwanariadha wa Kenya bingwa wa Olimpiki katika mashindano ya marathon, Eliud Kipchoge ametunukiwa tuzo ya kitaifa ya rais uhuru Kenyatta. Rais Kenyata ambaye anaongoza sherehe za Mashujaa Day mjini Mombasa pwani ya Kenya amemsifu mwanariadha huyo kwa kuwa mtu wa kwanza kuwahi kukimbia kilomita 42 chini ya saa mbili mjini Vienna. Rais Kenyatta amesema, tuzo ya mashujaa wote, waliopita, wa sasa na wajao, inamuendea Eliud Kipchoge. Rais pia alimtambua mwanariadha Brigid Kosgei ambaye hivi karibu alivunja rekodi ya wanawake ya mbio za marathon mjini Chicago.