Timu ya taifa ya Raga ya wachezaji saba kila upande ya Kenya inaangazia sasa Kombe la Afrika katika mashindano yatakayofanyika mwezi ujao baada ya kunyakua taji la Tusker Safari Sevens wikiendi iliyopita jijini Nairobi. Vijana hao wako katika mapumziko mafupi kabla ya kuanza tena mazoezi kwa ajili ya mashindano ya Kombe la Afrika yatakayofanyika Novemba 8 – 9 katika uwanja wa Bosman jijini Johannesburg, Afrika Kusini. Kenya imetwaa ubigwa wa Afrika katika mchezo wa Raga mwaka 2004, 2008, 2013, na mwaka 2015.