Abdirahman amesema serikali imepiga hatua kwenye mazungumzo ya kusamehewa madeni na maafisa wa Marekani, Uingereza, benki ya dunia na shirika la fedha duniani IMF.
Amesema Marekani imeonesha nia ya kuisamehe Somalia deni lake kwa kuzingatia utendaji wa kuridhisha wa Mogadishu kuelekea msamaha huo.
Jumamosi IMF ilielezea kuunga mkono Somalia kusamehewa madeni hivi karibuni.
Somalia inadaiwa dola bilioni 4.7 na IMF imesema kuwa nchi hiyo haiwezi kumudu kulipa au kuendelea kukopa zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |