• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Vituo vya jeshi kutumia kawi ya jua

    (GMT+08:00) 2019-10-23 19:53:54
    Taasisi na kambi zote za kijeshi, nchini Uganda katika siku za usoni zitatumia nishati ya jua katika hatua ya kupunguza gharama ya mabilioni ya pesa kwa Wizara ya Ulinzi.

    Kulingana na Waziri wa Ulinzi, Bwana Adolf Kasaija Mwesige, moja wapo wa gharama kubwa za oparesheni zimekuwa ni bili za umeme.

    Ili kufanikisha matumizi ya kawi ya jua wizara hiyo imeipa kampuni yaNexus Green kandarasi ya kutekeleza mradi wa majaribio ambao baada ya kufanikiwa unatarajiwa kuzalisha kilowati 516.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako