Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia uratibu wa mambo ya binadamu OCHA imetoa ripoti ikisema, takriban watu milioni 7.8 nchini Ethiopia wameendelea kuhitaji misaada ya kibinadamu katika muda uliobaki wa mwaka huu. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, dola bilioni 1.064 za kimarekani zinahitajika, lakini bado kuna pengo la dola milioni 319. Ripoti hiyo inasema serikali ya Ethiopia na wadau wengine wa mambo ya kibinadamu wamejitahidi kukabiliana na changamoto za ukame unaokabili sehemu za mashariki na mashariki kusini, mafuriko yaliyotokea katika baadhi ya maeneo nchini humo, na mahitaji ya kibinadamu kwa watu waliopoteza makazi, waliorudi na jamii za kuwapokea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |