Jumuiya ya maendeleo ya kusini mwa Afrika SADC imesisitiza tena wito wake wa kuondolewa vikwazo dhidi ya Zimbabwe.
Katibu mtendaji wa jumuiya hiyo Bw. Lawrence Tax ametoa taarifa ikisema, kuondoa vikwazo hivyo kutawanufaisha watu wa Zimbabwe, kanda ya SADC kwa ujumla na ushirikiano wake na Umoja wa Ulaya na Marekani.
Vikwazo hivyo vilivyowekwa mwaka 2002 na Marekani, Uingereza na Umoja wa Ulaya, ambavyo ni pamoja na vizuizi vya kibiashara, kuondoa uungaji mkono wa fedha wa pande mbili na nyingi, na vinakadiriwa kuigharamu Zimbabwe karibu dola bilioni 100 za kimarekani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |