Ujumbe wa ngazi ya juu unaowakilisha tume ya uchaguzi ya Palestina umewasili Gaza kwa ajili ya mazungumzo na kundi la Hamas kuhusu uchaguzi wa Palestina. Hapo awali, mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Palestina Bw. Hanna Nasser na ujumbe wake walitumwa na rais wa Palestina Bw. Mahmoud Abbas kutembelea Ukanda wa Gaza na kufanya mazungumzo na kundi la Hamas na vyama vingine vidogo vya nchi hiyo, kuhusu kufanya uchaguzi wa Palestina.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |