Wizara ya mambo ya ndani ya Tunisia imetangaza kuwa mamlaka ya Tunisia imevunja majaribio ya uhamiaji haramu wa kuvuka Bahari ya Mediterranean kuelekea Pwani ya Italia. Kwa mujibu wa wizara hiyo, majaribio hayo yalivunjwa na vikosi vya walinzi wa pwani vya mji mkuu wa Tunis, na majimbo ya Ariana, Mahdia na Monastir. Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo imesema, watu 48 wenye umri kati ya miaka 20 hadi 54 walikamatwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |