Granit Xhaka ameweka rehani unahodha wake baada ya kuibuka mzozo baina yake na mashabiki wa Arsenal. Mchezaji hiyo alifanya tukio hilo katika mchezo wa Ligi Kuu England ambao Arsenal alilazimishwa sare ya mabao 2 – 2 dhidi ya Crystal Palace. Xhaka alionyesha utovu wa nidhamu kwa mashabiki alipokuwa akitoka nje kumpisha mchezaji mwingine, na kuonyesha ishara isiyofaa kwa mashabiki ambao walimjibu kwa kumzomea.