• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Serikali ya Tanzania kushughulikia changamoto zinazowakabili wafanyabishara na wawekezaji katika bandari kuu ya Dar es Salaam

    (GMT+08:00) 2019-10-28 18:50:25

    Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano nchini Tanzania Isack Kamwelwe amesema, mipango inaendelea ya kuunda kikosi kazi kitakachosaidia kushughulika na changamoto zinazowakabili wafanyabiasharaa na wawekezaji katika bandari kuu nchini humo ya Dar es Salaam.

    Waziri Kamwelwe amesema kikosi kazi hicho kitaundwa na idara 22 zinazohusika na bandari hiyo, na kuongeza kuwa Tanzania iko makini katika kuvutia wafanyabiashara na wawekezaji kutumia bandari hiyo, jambo litakalofanikiwa kwa kumaliza changamoto zinazoikabili bandari hiyo.

    Amesema serikali imekuwa ikijitahidi kuboresha ufanisi wa bandari hiyo, ambayo ni mmoja kati ya bandari tatu zilizopo nchini humo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako