• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda: Kampuni za Wachina zimeandaa maonyesho ya Kazi kwa Vijana wa Rwanda

    (GMT+08:00) 2019-10-28 19:31:55

    Ubalozi wa China nchini Rwanda umeandaa maonyewsho ya kazi ya kwanza ya Wachina nchini Rwanda, ikilenga kutoa fursa za ajira kwa Wanyarwanda waliomaliza kutoka China.

    Hivi sasa kuna mamia ya Warwanda ambao wamehitimu kutoka taasisi za China katika taaluma tofauti.

    takriban kampuni 25 za Wachina zilizo chini ya Chama cha wafanyibishara cha Wachina nchini Rwanda walikutana mjini Kigali na Wanyarwanda wapatao 200 ambao walihitimu kutoka taasisi za China kwa maonyesho ya kazi.

    Akiongea katika hafla hiyo, Wang Jiaxin, Mshauri wa Uchumi na Biashara katika Ubalozi wa China nchini Rwanda, amesema kuwa hatua hiyo ilikuwa mawazo ya ubalozi wa China nchini Rwanda.

    Wang aliahidi fursa za maendeleo ya kazi na mishahara ya ushindani kwa wale ambao wamejiunga na biashara za Wachina.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako