Juma lililopita, ndge ya inayomilikiwa na serikali ya Zimbabwe ilifungiwa kupaa kutoka uwanja wa ndege wa Johannesburg baada ya kushindwa kulipia huduma za uwanja wa ndege. Kwa mjibu wa usimamizi mkuu wa uwanja wa ndege wa Johannesburg, hali hii ilitatuliwa siku ya Ijumaa iliyopita, baada ya Zimbabwe kulipa deni lake lote. Air Zimbabwe inapaswa kulipa ada ya kutumia viwanja vya ndege, kupakia ndege na huduma kwa wateja wake nchini Afrika kusini mara moja kwa wiki. Malipo haya yanapeanwa kwa shirika la kusimamia viwanja vya ndege nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |