Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO limetoa tahadhari kuhusu uwezekano wa kutokea kimbunga kaskazini mwa Somalia, zaidi ya mwaka mmoja baada ya kimbunga kingine kusababisha uharibifu mkubwa katika sehemu hiyo.
Kimbunga hicho kilichopewa jina la Kyarr kinatarajiwa kusababisha upepo mkali na mvua katika majimbo ya Puntland na Somaliland. Tahadhari inasema kimbunga hicho kinajikusanya kwenye bahari ya Hindi na kinatarajiwa kufika kwenye majimbo hayo kati ya siku nne na tano.
FAO imesema kuna umuhimu wa kuchukua hatua za lazima za tahadhari kwa kuwa upepo mkali unaweza kusababisha uharibifu wa miundo dhaifu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |