Mamlaka ya Utabiri wa Hali ya Hewa ya Tanzania TMA imetoa tahadhari kuhusu mikoa minne kwenye eneo la Ziwa Viktoria ikiwa ni pamoja na Simiyu ya Magharibi, Mara, Geita na Kagera, kukabiliwa na mvua kubwa wiki hii. TMA imetoa tahadhari hiyo wakati kuna ripoti kwamba watu zaidi ya 44 wamekufa katika sehemu nyingine nchini Tanzania kutokana na mvua zinazoendelea nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |