Ndege ndogo ya Marekani ilianguka katika jimbo la New Jersey, kaskazini mashariki mwa Marekani, na kusababisha nyumba zaidi ya moja kuwaka moto. Hali ya rubani bado haijajulikana. Mamlaka ya usafiri wa angani nchini Marekani FAA imesema itaanzisha uchunguzi, na Bodi ya Usalama wa Uchukuzi NTSB pia itashiriki kwenye uchunguzi huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |