Wataalam wanaohudhuria kongamano la kwanza la washauri bingwa wa China na Sudan Kusini lililofanyika mjini Juba, wamesema, mawasiliano yanayoongezeka kati ya Sudan Kusini na China ni muhimu kwa mustakabali wa maendeleo ya siasa, uchumi na miundombinu ya nchi hiyo.
Mkurugenzi wa taasisi ya utafiti kuhusu Afrika ya Chuo Kikuu cha Zhejiang, China, Bw. Liu Hongwu amesema, Sudan Kusini inaweza kujifunza mengi kutoka China katika mapambano dhidi ya umaskini, maendeleo ya uchumi na kuvutia uwekezaji kutoka nje. Amesema, ushirikiano kati ya China na Afrika hasa katika mafunzo na ujenzi wa miundombinu ni muhimu na unaweza kulifanya bara la Afrika, hususan Sudan Kusini, kujiendeleza kwa kasi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |