Ripoti ya aliyekuwa mkaguzi wa hesabu za serikali Edward Ouko katika mwaka wa kifedha uliokamilika Juni 2018 ilibainisha kwamba, NHIF ilitumia pesa hizo lakini ikakosa kuonyesha stakabadhi za kuthibitisha matumizi hayo.
Kulingana na stakabadhi zilizopelekwa mbele ya kamati ya uwekezaji katika Bunge la Kitaifa, kati ya fedha hizo, Sh13,115,573 zilitumika kuandaa warsha na makongamano.
Ingawa usimamizi umefafanua kwamba pesa hizo zilitumika kugharimia mikutano ya bodi, hakukuwa na ushahidi kuthibitisha matumizi hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |