Kamishna wa Amani na Usalama wa Umoja wa Afrika Bw. Smail Chergui, amesema licha ya maendeleo yaliyopatikana katika ngazi ya kitaasisi, mageuzi na utawala wa sekta ya usalama bado havijahusishwa kikamilifu katika majadiliano ya kukinga na kutatua migogoro ya Afrika.
Amesema kutokana na changamoto zinazoletwa na migogoro ya kisiasa na vizuizi vinavyotokana na changamoto hizo kwa maendeleo ya kisiasa, kijamii na kiuchumi, sasa ni wakati mwafaka kufanya mageuzi na utawala juu ya sekta ya usalama ambacho ni chombo cha ufumbuzi wa migogoro.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |