Ripoti ya mwaka ya Shirika la Fedha la Kimataifa IMF kuhusu makadirio ya uchumi wa kikanda iliyotolewa jana Alhamisi mjini Addis Ababa, inasema ukuaji wa uchumi wa kanda ya Afrika Kusini mwa Sahara unatarajiwa kuongezeka hadi kufikia asilimia 3.6 mwaka kesho kutoka asilimia 3.2 ya mwaka huu.
Akizindua ripoti hiyo mkurugenzi wa Kitengo cha Afrika cha IMF Bw. Papa N'diaye, amesema ukuaji wa uchumi unatarajiwa kuwa mzuri na kufikia wastani wa asilimia 6 katika nchi zisizotegemea maliasili, huku ukuaji ukikadiriwa kupungua katika nchi zinazotegemea maliasili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |