Mkutano wa 4 wa baraza la ngazi ya juu la vyombo vya habari vya nchi za BRICS ikiwa ni pamoja na Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini umefanyika jana mjini San Paulo, Brazil, na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka vyombo 55 vya habari vya BRICS.
Wajumbe hao wamejadiliana kwa kina mada mbalimbali ikiwemo kazi ya vyombo vya habari katika kuhimiza ushirikiano wa BRICS na dunia yenye ncha nyingi, na maendeleo ya teknolojia ya vyombo ya habari vipya kusaidia ushirikiano wa vyombo vya habari vya BRICS.
Mkutano huo pia umepitisha "mpango wa utekelezaji wa baraza la ngazi ya juu la vyombo ya habari vya BRICS".
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |