• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri mkuu wa China awasili Bangkok na kuhudhuria mikutano ya viongozi kuhusu ushirikiano wa nchi za Asia Mashariki

    (GMT+08:00) 2019-11-03 18:03:55

    Waziri mkuu wa China Bw Li Keqiang amewasili Bangkok jana usiku, ambako atahudhuria mkutano wa 22 wa viongozi kati ya China na Jumuiya ya nchi za Asia Kusini Mashariki ASEAN, mkutano wa 22 wa viongozi kati ya China, Korea Kusini, Japan na ASEAN, na mkutano wa 14 wa wakuu wa nchi za Asia Mashariki, na kufanya ziara rasmi nchini Thailand.

    Bw. Li amesema China inataka mikutano hiyo ifuatilie mambo ya ushirikiano wa kiutendaji, utaratibu wa dunia yenye ncha nyingi, biashara huria, kutatua masuala kupitia mazungumzo, kulinda amani na utulivu wa kanda, kuunga mkono kukuza uchumi, kuboresha maisha ya watu, na kuhimiza ushirikiano wa Asia Mashariki upate maendeleo zaidi.

    Aidha ameongeza kuwa anataka ziara hiyo ihimize zaidi urafiki kati ya China na Thailand, kuimarisha ushirikiano wa kunufaishana, na kuhimiza uhusiano wa wenzi wa ushirikiano wa kimkakati wa pande zote upate maendeleo mapya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako