Bondia Anthony Joshua anatarajiwa kuongeza mamilioni ya fedha baada ya pambano lake dhidi ya Andy Ruiz Jr litakalofanyika Desemba 7, mwaka huu nchini Saudi Arabia. Pamoja na hivyo, Joshua, bingwa wa zamani wa mikanda ya uzito wa juu ya WBA, WBO na IBF, bado yuko nyuma kwenye suala la utajiri kwa mabondia kwa kuwa ameachwa mbali na bondia mstaafu na nguli, Floyd Mayweather. Joshua atapanda ulingoni katika pambano hilo la marudio baada ya kupoteza awali kwa mpinzani wake huyo.