Dk. Shein aliyasema hayo jana Ikulu mjini Zanzibar alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania, Cho Taeick.
Katika mazungumzo hayo, Dk. Shein alimweleza Balozi huyo kuwa Zanzibar imeweza kuimarika katika sekta ya utalii kutokana na vivutio kadhaa vilivyopo sambamba na mikakati madhubuti iliyowekwa.
Aliongeza kuwa katika kuhakikisha uhusiano na ushirkiano unaimarika zaidi kati ya pande mbili hizo hasa katika sekta ya utalii, iko haja ya kuwapo ushirikiano kati ya Zanzibar na kisiwa cha Cheju nchini Korea ambacho ni maarufu duniani kwa utalii.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |