• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yatuma ujumbe kushiriki kwenye mkutano wa pili wa uwekezaji wa Afrika Kusini

    (GMT+08:00) 2019-11-07 08:49:48

    Kaimu balozi wa China nchini Afrika Kusini Bw. Li Nan jana huko Johannesburg aliandaa tafrija na kuukaribisha ujumbe wa uchumi na biashara wa serikali ya China utakaoshiriki kwenye mkutano wa pili wa uwekezaji nchini Afrika Kusini, utakaowakutanisha wajasiriamali na wajumbe wa mashirikisho ya biashara kutoka nchi hizo mbili.

    Bw. Li amesema China imetuma ujumbe wa ngazi ya juu wa serikali pamoja na wajasiriamali wengi kushiriki kwenye mkutano huo, ili kuunga mkono sera ya serikali ya Afrika Kusini kuongeza uwekezaji na nafasi za ajira. Hatua hii inaonesha imani ya China kwa maendeleo na ustawi wa Afrika Kusini na kuzidisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako