Watu wasiopungua 11 wakiwemo polisi wawili wameuawa katika mashambulizi ya ujambazi yaliyotokea kaunti ya Marsabit, kaskazini mwa Kenya. Kamanda wa polisi wa Marsabit, Bw. Steve Oloo amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na kusema hali ya wasiwasi inaendelea kuongezeka katika maeneo ya Jaldesa na Kukuto, karibu na mipaka ya Ethiopia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |