Maonyesho hayo,ambayo yameingia makala ya 10 sasa tangu kuanzishwa,yalifunguliwa jana nchini Uholanzi ,huku Rwanda ikishirikia kwa mara ya tatu sasa.
Uholanzi ndio soko kuu la maua duniani na kwa kiasi kikubwa mchangiaji mkuu wa mauzo ya nje ya maua ya Rwanda (asilimia 98).
Maonyesho hayo ya siku tatu yanaileta pamoja sekta ya maua duniani, ,huku yakilenga kuongeza uzalishaji na matumizi.
Mwaka huu Rwanda inashiriki ikiwa na malengo ya kukuza sekta ya maua ya nchi hiyo.Matokeo yaliyokusudiwa ni athari chanya kwa mauzo na mahitaji ya maua ya Rwanda kupitia soko la mnada wa maua la Uholanzi.
Sekta ya maua nchini Rwanda katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni imekua na kuvutia wawekezaji na soko kutokana na fursa na viungo vya soko kwa ajili ya bidhaa hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |