Shirika la Afya Duniani WHO limesema mafuriko yamesababisha vifo vya watu wasiopungua 25, na wengine 47 kujeruhiwa kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha. WHO inasema mvua kubwa imeathiri sehemu nyingi za Somalia na kusababisha watu zaidi laki 2.7 kupoteza nyumba zao na kuvuruga uzalishaji na kuharibu miundombinu nchini humo. Shirika hilo limechukua hatua za dharura ili kuokoa maisha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |