Rais Paul Biya wa Cameroon jana alisaini amri ya rais akitangaza kuwa uchaguzi wa wabunge na madiwani utafanyika tarehe 9 mwezi Februari mwaka kesho.
Uchaguzi huo uliahirishwa mara mbili kutokana na matishio ya watu wenye silaha yaliyoongezeka kwenye maeneo mawili yanayotumia lugha ya Kiingereza, na mashambulizi ya kundi la Boko Haram kwenye mkoa wa kaskazini wa nchi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |