Meneja mtendaji wa Mamlaka ya mawasiliano ya Tanzania TCRA Bw. Semu Mwakyanjala amesema, watu milioni 12 tu kati ya jumla ya milioni 43.75 waliosajili simu za mkononi wameandikisha kadi zao za SIM kwa njia ya mfumo wa kibiometrika, na simu zao ziko hatarini ya kufungwa tarehe 31 Desemba ikiwa ni tarehe ya mwisho ya usajili. TCRA ilitoa maelekezo mwezi Mei mwaka huu kusajili kadi za SIM kwa njia ya kibiometrika kabla ya mwishoni mwaka huu, hatua ambayo inalenga kuwaondoa watumiaji wasio waaminifu, na kudhibiti uhalifu wa mtandaoni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |