• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • AU yapongeza ushirikiano kati yake na Umoja wa Mataifa kwenye ulinzi wa amani na usalama barani Afrika

    (GMT+08:00) 2019-11-13 08:12:24

    Umoja wa Afrika jana umepongeza uhusiano uliopo kwenye ulinzi wa amani na usalama kati ya Kamisheni ya Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa.

    Taarifa hiyo imetolewa na kamishna wa Umoja wa Afrika anayeshughulikia amani na usalama Bw. Smail Chergui, kwenye mkutano kati ya kamisheni ya kujenga amani ya Umoja wa Mataifa na Baraza la amani na usalama la Umoja wa Afrika.

    Amesema ushirikiano kati ya Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa umepata matokeo katika nchi mbalimbali za Afrika, zikiwemo Jamhuri ya Afrika ya Kati, Sudan, Sudan Kusini, Somalia, Madagascar na Mali, na unaweza kuimarishwa zaidi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako