• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • MAGARI: Janga la moto lasababisha World Rally Championship kuahirishwa nchini Australia

    (GMT+08:00) 2019-11-13 08:12:49

    Raundi ya mwisho ya mashindano ya magari ya World Rally Championship yameahirishwa kwasababu ya tishio la moto nchini Australia. Rally Australia ilipangwa kufanyika wikiendi hii huko New South Wales. Watu watatu wamekufa na zaidi nyumba 150 zimeteketea siku ya ijumaa. Mwenyekiti wa kamati ya maandilizi ya Rally Australia Andrew Papadopoulos amesema wamechukua uamuzi huo wakiangalia maslahi na usalama wa kila mtu. Hali ya dharura imetangazwa kwa siku saba huku mamlaka zikionya kwamba moto unaweza kusambaa haraka kutokana na hali ya joto na upepo mkali.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako