Pato la ndani la Tanzania GDP limeongezeka kwa asilimia 7.2 katika robo ya pili ya mwaka huu, ikilinganishwa na asilimia 6.1 ya mwaka jana wakati kama huo.
Benki kuu ya Tanzania BoT imesema sekta muhimu zilizochangia zaidi ongezeko la uchumi ni ujenzi, kilimo na madini, ambazo zimechangia asilimia 67.7 ya ukuaji huo.
Shughuli zenye ongezeko la kasi zaidi ni ujenzi, ambazo ongezeko lake lilikuwa asilimia 19.6, na mfumuko wa bei uko chini ya asilimia 5, ambalo ni lengo la muda wa kati la nchi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |