Mkurugenzi wa Hospitali ya mafunzo nchini Sudan Kusini Bw. Isaac Cleto amesema mradi wa miundombinu ya afya wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 33 unaofadhiliwa na China nchini Sudan kusini utaboresha utoaji wa huduma za afya nchini humo. Bw. Cleto amesema kipindi cha kwanza cha mradi huo ambacho ni pamoja na ujenzi wa wodi za kisasa za dharura na za uzazi unatarajiwa kukamilika katika siku za usoni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |