Umoja wa Mataifa umetoa dola za kimarekani milioni 18.7 ili kuimarisha utoaji wa msaada kwa watu zaidi ya laki 5 walioathirika na mafuriko nchini Somalia. Mratibu wa mambo ya kibinadamu nchini Somalia Bw. Adam Abdelmoula amesema fedha hizo zinatolewa kwa wakati muhimu, na zinawawezesha wenzi wa mambo ya kibinadamu kuongeza utoaji wa misaada kwa waathirika wa mafuriko wanaohitaji makazi, maji safi, chakula na huduma za matibabu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |