Chama cha upinzani cha Umoja wa Demokrasia cha Afrika Kusini DA kimemteua Bw. John Steenhuisen aliyeahidi kustawisha tena chama hicho kuwa kiongozi wake wa muda. Bw. Steenhuisen aliyekuwa kiongozi wa bunge wa chama cha DA amemshinda mpinzani wake Bw. Makashule Gana kwa kupata asilimia 75 ya kura. DA imekosa kiongozi tangu mwezi Oktoba Mmusi Maimane kujiuzulu kutokana na mvutano wa ndani. Kiongozi wake rasmi atachaguliwa mwezi Aprili mwakani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |