Serikali ya Ethiopia imesema Wabrazil watano wamekamatwa kwa kutuhumiwa kujaribu kufanya magendo ya Cocaine kilo 47.4 kwa nchi kadhaa kupitia Ethiopia. Habari zilizotolewa na Shirika la Utangazaji la FANA zinasema, Cocaine hiyo ilikamatwa katika Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Bole mjini Addis Ababa, na kati ya watu waliokamatwa, wanne ni wanawake. Habari zinasema watuhumiwa watatu kutoka Brazil walikuwa wakielekea Kigali kupitia Addis Ababa, na wengine wakielekea Johannesburg, Afrika Kusini, na Bangkok, Thailand.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |