• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • E-Sokoni yalia changamoto ya elimu kwa wakulima

    (GMT+08:00) 2019-11-18 19:16:53
    Jukwaa la Kidigitali la kuwasaidia wakulima na wafanyabiashara kupata taarifa za kilimo na masoko (E-Sokoni) limesema bado kuna changamoto ya kukosa elimu na taarifa kwa wakulima jambo ambalo husababisha hasara kwa kukosa masoko na mazao kuharibikia shambani.

    Mwanzilishi wa Jukwaa hilo, Edrick Mashamba amesisitiza kuwa jukwaa hilo ni ukombozi kwa wakulima na wafanyabiashara wa mazao katika kupata taarifa zitakazopelekea kupunguza au kuondoa kabisa hasara pamoja na urasimu.

    Aliongeza kuwa E-Sokoni imedhamiria kuipa thamani sekta ya kilimo kwa kufanya wakulima kujivunia pamoja na kurahisisha maisha ya Mtanzania kupata chakula kwa urahisi na bei rafiki.

    Alisema kuwa jukwaa hilo ni fursa kwa maafisa ugani kwani litawasogeza karibu na wateja na kuwaondolea gharama za ziada huku akiomba serikali kupitia Wizara ya Kilimo kuwaunga mkono kuifanya sekta ya kilimo kuwa na manufaa kwa kila mtu anayejihusisha nayo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako