Rais wa zamani wa Uefa Michel Platini ameponda matumizi ya VAR, teknolojia ambayo kila samesema teknolojia hiyo inachukua nusu saa zima kuelezea kwanini haikutatua tatizo. Platini mwenye miaka 67 alikuwa kinyume na matumizi ya teknolojia hiyo ambayo alikataa kuizingatia baada ya kuwa rais wa Uefa chief mwaka 2007. Mwaka huu pia Uefa imetambulisha matumizi ya teknolojia ya kuchezesha tena video katika Ligi ya Mabingwa mwaka huu. Wakati huohuo nyota huyo wa zamani wa Juventus anaamini kuwa bado anaweza kubeba jukumu kwenye soka baada ya kusimamishwa kwa miaka mine kushiriki michezo adhabu ambayo imeisha Oktoba. Alisimamishwa na Fifa mwaka 2015 kwa malipo aliyopokea kwa njia ya utata kiasi cha Sh204 million ($2 million) alizopata kutoka kwa Blatter. Na amekuwa akikanusha kuwa hakufanya kosa lolote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |