• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Afrika Kusini yasisitiza kuondolewa kwa vikwazo dhidi ya Zimbabwe

    (GMT+08:00) 2019-11-19 08:59:03

    Waziri wa mambo ya nje wa Afrika Kusini anayeshughulikia uhusiano na ushirikiano wa kimataifa Bibi. Naledi Pandor, ametoa wito tena kuondolewa kwa vikwazo vya Marekani na Umoja wa Ulaya dhidi ya Zimbabwe. Bibi Pandor amesema hayo katika kongamano la kujadili njia bora ya kutimiza ustawi wa Zimbabwe lililofanyika huko Pretoria.

    Bibi Naledi amesema vikwazo hivyo vinachochea msukosuko na hali mbaya ya kijamii nchini Zimbabwe, lakini pia vimeiathiri vibaya Afrika Kusini, na hata bara la Afrika, kwa hiyo vinapaswa kuondolewa ili kuhimiza maendeleo ya Zimbabwe.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako