• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • BASKETBALL: Bandari, Storms watia fora vikapuni

    (GMT+08:00) 2019-11-19 17:15:19
    Timu za mpira wa vikapu za Bandari na Storms za Kenya zimeingia nusu-fainali ya Ligi Kuu ya wanawake baada ya kung'aa katika robo-fainali jijini Nairobi, wikendi. Bandari waliwabanjua wenyeji wao Eagle Wings 2-0 katika mfululizo wa mechi tatu za robo-fainali. Ilifunga Wings 78-43 katika mechi ya kwanza Jumamosi. Bandari, ambayo ilipoteza ubingwa kwa kulazwa 3-1 dhidi ya Equity Bank katika fainali ya mwaka jana, haikulegeza kamba katika mechi ya pili ambapo ililaza Wings 79-31 Jumapili. Storms,iliyokamilisha msimu wa kawaida katika nafasi ya sita, ilianza robo-fainali kwa kushindwa 42-39 na Strathmore. Hata hivyo, Storms ya kocha Abel Nson iliamka katika mechi ya pili na kushinda 70-54. Storms ilimaliza katika nafasi ya tatu mwaka jana.
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako