Akiwasilisha mada ya mgawanyo wa mapato ya mafuta katika mafunzo kuhusu mafuta na gesi asilia kwa wanasheria wa serikali, Mshauri Mwelekezi wa Mafuta na Gesi, Yona Killagane, alisema uchimbaji wa mafuta unatumia fedha nyingi, hivyo bila kuwa na uamuzi wenye maslahi ya taifa, unaweza kusababisha serikali kuingia hasara.
Killagana alisema nchi nyingi zinazoendelea zinaingia hasara kwa kukosa sera makini, hivyo kuwataka kufahamu majukumu yao katika kuhakikisha wanakuwa na mipango imara ya kulinda sekta hiyo.
Pia aliishauri Mamlaka ya Udhibiti na Utafutaji Mafuta na Gesi Asilia (ZPDC) kuhakikisha watakapopata mikataba ya kutafuta na kuchimba mafuta, isiingie katika mfumo wa kukodi majengo au vifaa kwa kuwa watakapomaliza watashindwa kunufaika na gharama zinazoweza kutumiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |