Mamlaka ya Palestina imeupongeza Umoja wa Mataifa kwa kutetea haki ya kujiamulia ya watu wa Palestina, na kuona hatua hii ni jibu la haraka dhidi ya kauli za waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Mike Pompeo kuwa ujenzi wa makazi ya wayahudi katika Ukingo wa Magharibi haukiuki sheria ya kimataifa. Kwenye mkutano wa Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, nchi 165 zilipiga kura ya kuunga mkono, nchi 5 zikikataa na tisa hazikupiga kura kuhusu azimio la kutetea haki ya kujiamulia ya wapalestina.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |