Jukwaa la kwanza la taifa la Video linalotumia mtandao wa 5G Yangshipin limezinduliwa rasmi.
Jukwaa hilo limebuniwa na Shirika Kuu la Utangazaji la China (CMG) juu ya msingi wa teknolojia ya mtandao wa 5G, video ya kiwango cha juu cha 4K na 8K na akili bandia. Uzinduzi wa jukwaa hilo unamaanisha hatua muhimu kwa kituo hicho katika muungano wa vyombo vya habari vya aina tofauti.
Mkuu wa CMG Bw. Shen Haixiong amehutubia katika hafla ya uzinduzi huo na kusema, shirika hilo litatumia nguvu bora ya vyombo vya habari vya redio na video vya taifa na kulifanya jukwaa hilo kuwa daraja la kuunganisha vyombo vikuu vya habari na watumiaji, kiongozi wa teknolojia mpya ya mtandao wa Internet, na msabazaji wa mitazamo muhimu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |