Bingwa wa Mbio za Nusu-Marathon Duniani, Geoffrey Kamworor ametambuliwa rasmi na Shirikisho la Riadha Duniani (IAAF). Rekodi yake ya awali ya 58:23 ilivunjwa na Zersenay Tadese jijini Lisbon mwaka 2010 lakini IAAF imesema rekodi hiyo kwa sasa inasalia kushikiliwa na Mkenya huyo. Katika kivumbi kikali cha kutetea taji hilo, Kamworor alishikilia rekodi hiyo kwa tofauti ya sekunde 22 wakati wa mbio za Copenhagen Half Marathon Septemba 15, ambapo aliweka rekodi mpya ya 58:01. Mwanariadha huyo alikaribia kuvunja rekodi ya muda wa dakika 58. Nguli huyo mwenye umri wa miaka 26 alishinda mataji yake matatu ya kwanza jijini Danish mwaka 2014.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |